Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe, amevamiwa na kushambuliwa na watu wasiojulikana wakati akirejea nyumbani kwake jijini dodoma.
Msemaji wa CHADEMA Tumaini Makene, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo lilitokea usiku wa Jumatatu, ambapo amevieleza vyombo vya habari kuwa kwa sasa anapokea matibabu.
Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika amevieleza baadhi ya vyombo vya habari kuwa shambulio hilo lina sura ya kisiasa, na amesema kuwa taarifa zaidi zitatolewa baadae.
Aidha, shambulio hili dhidi ya mwenyekiti wa CHADEMA linakuja siku moja baada ya mwanasiasa wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu kutangaza rasmi nia ya kuwania urais kupitia chama cha CHADEMA.