Star Tv

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefungua milango kwa wanachama wa chama hicho wanaotaka kugombea nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu kujitokeza kuanzia leo Juni 3 hadi Juni 15 mwaka huu.

Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, akiongea na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mnyika amesema taarifa za kusudio la kugombea urais kupitia chama hicho zinapaswa kuwasilishwa katika ofisi ya Katibu Mkuu na baadae zitajadiliwa na Kamati Kuu ya chama hicho na kutolewa uamuzi.

Kwa mamlaka niliyopewa na kanuni hii ya chama ninaomba kutangaza sasa tarehe za mwanzo wa zoezi hili na tarehe za mwisho wa zoezi hili la kutangaza nia ya kusudio la kugombea milango hii imefunguliwa kuanzia tarehe ya leo mpaka tarehe 15 ya mwezi Juni” amesema Mnyika

Licha ya suala hilo la kugombea nafasi ya urais Katibu Mkuu huyo pia amesema kuwa chama hicho kimefungua milango ya ushirikiano na vyama vingine kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu na vyama ambavyo ameviita ni vyama makini.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.