Mazishi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Ukerewe Marehemu Masoud Mohamed ambaye alijozolea umaarufu mkubwa mitandaoni baada ya video zake kusambaa akisoma Quran Tukufu yamefanyika leo alasiri mkoani Tabora.
Mazishi ya Marehemu Masoud mbali na kuhudhuriwa na ndugu, wafanyakazi wenzake na majirani pia baadhi ya viongozi wa Serikali na wa Dini walihudhuria mazishi hayo akiwemo mwakilishi wa Mufti Mkuu nchini.
Marehemu Masoud ni mmoja wa Maaskari waliobadilishwa vituo vya kufanyia kazi hivi karibuni akitokea kituo cha kazi cha Bunda Mkoani Mara.
Marehemu alikutwa na umauti Mei 08, akiwa hotelini mahali alipofikia wakati ameripoti kwenye kituo chake kipya cha kazi Wilayani Ukerewe ambapo alikuwa akiishi baada yakukosa nyumba na hivyo alikuwa akitekeleza majukumu yake wakati anasubiri kutafutiwa nyumba ya kuishi.