Star Tv

Katika kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano inayohimiza uchumi wa viwanda, jeshi la Polisi nchini limetakiwa kuwahimiza askari wake kujikita katika masuala ya ujasiriamali ili kuyafikia maendeleo yanayotokana na biashara kwa kupatiwa mafunzo na elimu ya ujasiramali.

Ujasiriamali na biashara ni jambo linalohimizwa kwa kila mtanzania mwenye utimamu wa akili, na lengo kuu likiwa ni kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na hata Taifa kwa ujumla- ambapo jeshi la Polisi - askari wake wametakiwa kutojiweka kando na badala yake wachangamkie fursa za kibiashara.

Julius Mjengi ni kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa , naye anaona suala ujasiriamali ndiyo wimbo unaopaswa kuimbwa kwa pamoja kwa kila mtanzania wa Taifa hili.

Rai hii imetolewa katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya mtandao wa Polisi wa kike mkoani Iringa, shughuli ambayo Rita Kabati mbunge wa Viti maalumu CCM mkoani Iringa ndiye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hii.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.