Mkuu wa Jeshi ka Zimamoto na Uokoaji Kamishna Jenerali John Masunga amesema tayari wametekeleza agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kijana aliyesaidia katika shughuli za uokoaji kwenye ajali ya ndege ya shirika la presicion iliyotokea Novemba 06, 2022 wilayani Bukoba mkoani Kagera kwamba tayari wameshampokea Majaliwa Jackson Samweli kwa ajili ya kuanza mafunzo.
Masunga amesema kijana huyo anatarajiwa kuanza mafunzo ya Zimamoto na uokoaji pamoja na uaskari katika Chuo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kilichopo Chogo wilayani Handeni mkoani Tanga.
Aidha Masunga ametoa wito kwa wananchi wote kuendelea kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika kuokoa maisha ya watu na mali dhidi ya majanga mbalimbali.