Star Tv

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa Baraza la Mitihani ya Taifa limejiridhisha kwamba watahiniwa katika shule ya Chalinze Modern Islamic walibadilishiwa namba ya mtihani.

Kauli hii ya Waziri inakuja siku chache baada ya video zilizosambaa katika mitandao zikimuonesha mtahiniwa katika Shule ya Awali na Msingi Chalinze Modern Islamic Iptisum Suleiman Slim akilalamikia kubadilishiwa namba ya mtihani wa darasa la saba.

Prof. Mkenda amesema baada ya uchunguzi imebainika kuwa ni kweli mtahiniwa alibadilishiwa namba na kwamba pia watahiniwa wengine saba walibadilishiwa namba za mtihani.

Aidha kutokana na kukutwa na kosa hilo Serikali imeifungia shule hiyo kuwa kituo cha mitihani kwa muda usiojulikana kutokana na taarifa ya Kamati ya Mitihani ya Mkoa wa Pwani pamoja na taarifa ya Wataalamu wa Miandiko kutoka Jeshi la Polisi kubainika kuwa Watahiniwa 7 akiwemo Iptisam walibadilishiwa namba za mtihani katika Shule hiyo.

Mkenda amesema uchunguzi uliofanywa na Kamati ya Mitihani ya Mkoa wa Pwani umebaini kuwa Mtahiniwa Iptisam Suleiman Slim alifanya masomo matano kwa kutumia namba PS1408009/0040 na somo la sita (mwisho) kwa kutumia namba PS1408009/0039.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.