Star Tv

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa Baraza la Mitihani ya Taifa limejiridhisha kwamba watahiniwa katika shule ya Chalinze Modern Islamic walibadilishiwa namba ya mtihani.

Kauli hii ya Waziri inakuja siku chache baada ya video zilizosambaa katika mitandao zikimuonesha mtahiniwa katika Shule ya Awali na Msingi Chalinze Modern Islamic Iptisum Suleiman Slim akilalamikia kubadilishiwa namba ya mtihani wa darasa la saba.

Prof. Mkenda amesema baada ya uchunguzi imebainika kuwa ni kweli mtahiniwa alibadilishiwa namba na kwamba pia watahiniwa wengine saba walibadilishiwa namba za mtihani.

Aidha kutokana na kukutwa na kosa hilo Serikali imeifungia shule hiyo kuwa kituo cha mitihani kwa muda usiojulikana kutokana na taarifa ya Kamati ya Mitihani ya Mkoa wa Pwani pamoja na taarifa ya Wataalamu wa Miandiko kutoka Jeshi la Polisi kubainika kuwa Watahiniwa 7 akiwemo Iptisam walibadilishiwa namba za mtihani katika Shule hiyo.

Mkenda amesema uchunguzi uliofanywa na Kamati ya Mitihani ya Mkoa wa Pwani umebaini kuwa Mtahiniwa Iptisam Suleiman Slim alifanya masomo matano kwa kutumia namba PS1408009/0040 na somo la sita (mwisho) kwa kutumia namba PS1408009/0039.

Latest News

Dkt. Jafo ofisi yake, imekamilisha taratibu zote za kupata Ithibati ya Kitabu ch...
24 Apr 2023 09:38 - Kisali Shombe

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo amewasilisha bungeni Hotuba ya Ma [ ... ]

TARI, Ukiruguru kuzindua Kifaa cha kupandia Mbegu cha Rafiki
23 Apr 2023 18:33 - Kisali Shombe

Sekta ya Kilimo ni mhimili wa uchumi wa Tanzania na imekuwa ikichangia Pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na Taifa kwa uj [ ... ]

Wanawake kuwa sehemu ya Elimu dhidi ya Itikadi Kali na Ugaidi Afrika.
17 Apr 2023 10:28 - Kisali Shombe

Mnamo Oktoba 14, 2017, Mogadishu, Somalia ilikumbwa na shambulio baya la kigaidi lililoua watu 587 na kujeruhi zaidi ya  [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.