Siku chache Baada ya CCM kushauri serikali kufuta tozo, pamoja na kelele za muda mrefu za Wananchi kuhusu tozo, Waziri wa Fedha na Mipango Dokta Mwigulu Nchemba ametangaza kufuta baadhi ya Tozo.
Tozo zilizofutwa ni pamoja na Miamala ya ndani ya Benki, Tozo ya kuhamisha Fedha kutoka Benki kwenda Mitandao ya simu, Miamala ya Benki Moja na nyingine na Miamala ya ATM isiyozidi Tsh. 30,000.
Vilevile Dkt. Nchemba amesema Serikali imepunguza kwa 10% - 50% Makato ya Miamala ya Simu na Miamala ya Benki kutegemea na makundi ya Miamala na Gharama zilizowekwa.
Aidha marekebisho hayo yataanza rasmi Tarehe ya kwanza ya mwezi Oktoba Mwaka huu wa 2022.