Star Tv

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Prof. Joyce Ndalichako amesema Serikali imedhamiria kutoa fursa kwa vijana nchini ili waweze kuondokana na changamoto ya ajira.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo wakati alipoambatana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria walipotembelea mradi wa Kitalu Nyumba (Greenhouse) katika Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa lengo la kukagua maendeleo ya mafunzo hayo ya kilimo cha kisasa yanayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

“Mheshimiwa Rais amedhamiria kutoa fursa zaidi kwa vijana nchini na serikali anayoiongoza imekuwa ikiwapatia vijana fursa mbalimbali ikiwemo ujuzi na stadi za kazi ili waweze kushiriki kwa ufanisi katika shughuli za uzalishaji mali sambamba na kuongeza fursa za ajira”- Waziri Ndalichako

Amesema kuwa, katika kufanikisha hilo Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imekuwa ikiratibu Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi ambayo imelenga kuwezesha nguvu kazi ya Taifa kupata ujuzi na stadi za kazi stahiki ili kumudu ushindani wa soko la ajira na kuwawezesha kujiajiri au kuajiri wenzao.

Aidha, Waziri Ndalichako ametoa wito kwa Viongozi wa Halmashauri kuhakikisha wanatekeleza maagizo ya Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa kwa kuwezesha vijana vitendea kazi kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani (4% Vijana, 4% Wanawake na 2% Watu wenye Ulemavu ili kuwawezesha vijana hao kufanya kazi au shughuli zenye tija.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.