Star Tv

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishina Msaidizi wa Polisi ACP. Justine Masejo leo Desemba 28.2021 ametoa taarifa juu ya tukio la mauaji ya marehemu Ruth Mmasi lililotokea mwishoni mwa wiki iliyopita mwaka huu 2021 huko maeneo ya Njiro katika halmashauri ya jiji la Arusha.

ACP. Masejo amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na linamshikilia mtu mmoja kwa mahaojiano ya kina juu ya tukio hilo ambalo lilipelekea umauti wa marehemu Ruth Mmasi.

Kamanda masejo ameendelea kusema kuwa mtuhumiwa ambae anatuhumiwa anaendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi na kupelekea kupata baadhi ya vielelezo kuhusiana na tukio hilo.

Ameeleza kuwa Chanzo cha tukio hilo bado kinachunguzwa na amewaomba wananchi, ndugu na jamaa kuwa wavumilivu wakati Polisi wakiendelea na uchunguzi wa kina kuhusiana na tuko hilo.

Ametoa wito kwa viongozi wa dini na makundi mbalimbali ya kijamii na kimila kuendelea kuelimisha wananchi kutojichukulia sheria mkononi, kitendo ambacho ni kinyume na sheria za nchi yetu.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.