Star Tv

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamshikilia mkazi mmoja wa Kijiji cha Ndungi katika Wilaya ya Moshi kwa tuhuma za kumuua ndugu yake, William Shoo kwa madai ya kukataa kuchangia nyama ya Shilingi 1,500 waliyonunua.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 11, 2021  amesema mauaji hayo yalitokea Oktoba 10, 2021 asubuhi baada ya marehemu kugoma kuchangia nyama hiyo waliyonunua.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, kabla ya mauaji hayo mtuhumiwa alinunua nyama kwa kushirikiana na marehemu ambapo walikula pamoja na walipomaliza kula marehemu alikataa kuchangia chochote ndipo ugomvi ukaanza.

Amesema katika ugomvi huo, mtuhumiwa alimkata ndugu yake na kitu chenye ncha kali kichwani na kusababisha kifo chake.

"Awali kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa alinunua nyama kwa kushirikiana na mwenzake, ambayo ina thamani ya Shil. 1,500 walipokula pamoja ndugu yake huyo alikataa kulipia, ndipo ugomvi ukaanza ambapo ilipelekea kuchukua maamuzi hayo ya kumkata na kitu chenye ncha kali"

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.