Star Tv

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wa serikali za mitaa kutoa elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa chanjo ya UVIKO-19 kwa wananchi.

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi hao kutotumia mabavu katika utoaji wa chanjo bali kuwaelimisha wananchi wapate chanjo kwa hiari.

Rais ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano mkuu maalum wa uchaguzi wa viongozi wa jumuiya ya serikali za mitaa ALAT Taifa Mkoani Dodoma.

“Tulisema hili jambo ni la hiari, ukipita nyumba kwa nyumba anayetaka mchome asiyetaka usichome Lakini kubwa ninalotaka kusema mtu ana hiyari ya kukubali au kukataa na kama ana elimu ya kutosha, hawezi kukataa”-Rais Samia Suluhu Hassan

Katika mkutano huo maalum Rais Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi hao kushirikiana na kuondoa tofauti Zao ambazo nyingi hutokana na maslahi binafsi.

Aidha, Rais Samia amewakumbusha viongozi hao kuhakikisha wanawatumikia wananchi vema kwa kutatua changamoto zao na si vinginevyo.

"Katika mkutano mmoja nilisema sitaki kuona mabango yenye masikitiko, yenye shukrani wacha wananchi waandike, mabango yenye masikitiko ni kwa sababu viongozi kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa hamfanyi kazi yenu, baadhi yenu ni sehemu ya kero".

Rais Samia Suluhu Hassan leo Septemba 27, ameshiriki mkutano mkuu maalum wa uchaguzi wa viongozi wa jumuiya ya tawala za mitaa tanzania (ALAT) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Center Jijini Dodoma.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.