Star Tv

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa amewapongeza vijana wa Timu ya Taifa Stars na Watanzania wote kwa ushindi wa Magoli 3 - 2 dhidi ya Timu ya Madagascar kwenye mchezo uliochezwa leo Septemba 07, 2021 wa Michuano ya kufuzu kombe la Dunia 2021.

Bashungwa ameeleza kuwa Wizara itawapa zawadi ya Tsh 10,000,000 kuwapongeza kwa jitihada safi ya mapambano ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2021.

Ushindi huo unaifanya Stars kuwa kileleni katika msimamo wa kundi J ikiwa na alama 4.

Mabao ya Stars yamefungwa na

  1. Erasto Nyoni-Penalti
  2. Novatus Dismasi
  3. Feisali Salum Abdallah

Aidha, Bashungwa ametoa wito kwa kuwaomba wadau wowote mwenye zawadi kwa Taifa Stars wawasiliane na Wizara ili kutambua zawadi ya michango hiyo ya hamasa kwa Taifa Stars.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.