Deprecated: Array and string offset access syntax with curly braces is deprecated in /var/www/html/startv.co.tz/public_html/startvweb/plugins/system/SEOSimple/SEOSimple.php on line 156

Deprecated: Array and string offset access syntax with curly braces is deprecated in /var/www/html/startv.co.tz/public_html/startvweb/plugins/system/SEOSimple/SEOSimple.php on line 156

Deprecated: Array and string offset access syntax with curly braces is deprecated in /var/www/html/startv.co.tz/public_html/startvweb/plugins/system/SEOSimple/SEOSimple.php on line 156

Deprecated: Array and string offset access syntax with curly braces is deprecated in /var/www/html/startv.co.tz/public_html/startvweb/plugins/system/SEOSimple/SEOSimple.php on line 157

Deprecated: Methods with the same name as their class will not be constructors in a future version of PHP; plgSystemSEOSimple has a deprecated constructor in /var/www/html/startv.co.tz/public_html/startvweb/plugins/system/SEOSimple/SEOSimple.php on line 15
WAZIRI BASHUNGWA AWAPA CHANGAMOTO MAKATIBU TAWALA.
Star Tv

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amewaagiza Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kasimu Majaliwa, kusimamia michezo katika ngazi zao ili kuwawezesha vijana kukuza vipaji vyao vya michezo kupitia sekta hiyo.

Waziri Bashungwa amewakumbusha viongozi hao kwa nyakati tofauti mwishoni mwa wiki alipofanya ziara ya kikazi na viongozi wa wilaya ya Biaharamulo mkoani Kagera na wilaya ya Bukombe mkoani Geita katika ligi mbili tofauti katika wilaya hizo.

Akizungumza katika vikao na viongozi ngazi ya wilaya, Waziri Bashungwa amesema Makatibu Tawala ndio wenye jukumu la kusimamia michezo kwa ngazi ya mikoa na wilaya ambapo wamepewa mamlaka hayo kupitia Sera ya Michezo ya mwaka 1995.

“Kwa mujibu wa Sera hiyo, hawa ndiyo wenyeviti wa kamati za michezo za ngazi ya mikoa na wilaya, hivyo wanawajibika moja kwa moja kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo”-Amesema Waziri Bashungwa.

Sambamba na hilo, Waziri Bashungwa ameliagiza Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kwa kushirikiana na Baraza la Michezo nchini (BMT) pamoja na Chuo cha Michezo cha Malya kuangalia uwezekano wa kuwawezesha walimu wa michezo kutoka katika chuo hicho kutembelea maeneo mbalimbali katika ngazi ya wilaya na vijiji kutoa elimu elekezi ya uamuzi wa mchezo wa soka nchini ili kujenga uelewa unaolenga kuleta tija kwa wachezaji na taifa kwa ujumla.

Akiwa ziarani katika mikoa ya kanda ya Ziwa, Waziri Bashungwa ameshiriki kufunga mashindano ya ligi mbili za ngazi ya wilaya ambazo ni “Engineer Ezra Cup” yaliyodhaminiwa na Mbunge wa jimbo Biharamulo mkoani Kagera Mhandisi Ezra Chiwelesa pamoja na mashindano ya “Doto Cup” yaliyodhaminiwa na Waziri wa Madini na Mbunge wa jimbo la Bukombe Mhe. Doto Biteko.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.