Waziri wa Fedha na Mipango nchini Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema tozo za miamala ya simu si michango ya kirafiki ni sheria iliyopitishwa na Bunge baada ya kujadiliwa kwa kina akibainisha kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi.
Dkt.Nchemba amezungumza hayo leo Ijumaa Agosti 20, 2021 katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
“Yaani inanyesha mvua moja tu mtoto inabidi alale shuleni hivi nani anaweza kumuamini jirani tu mtoto alale kila siku......niambie mzazi unalala usingizi wa aina gani, kuna vitu ni serious kweli kweli ambavyo wabunge wanavisemea ambavyo vinatulazimisha tufunge mikanda"- Dkt Mwigulu.
Aidha, waziri Mwigulu amesema kuwa fedha zilizopatikana baada ya ukusanyaji wa tozo tangu sheria ilipoanza kutumika mwezi mmoja uliopita, zimetumika kuboresha sekta ya afya, elimu na miundombinu.