Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema John Mnyika amesema kamati kuu ya chama hicho itakaa Julai 22 mwaka huu ili kujadili ni maelekezo gani kama chama wanapaswa kutoa kwa wanachama ya kumtafuta mwenyekiti wao, Freeman Mbowe, ambaye hajulikani alipo mpaka sasa.
Akizungumza na wanahabari Mnyika amesema kama chama hawafamu mwenyekiti wao Freeman Mbowe alipo na kuwaomba wananchi wasaidie kumtafuta
Mnyika amewaomba viongozi na wanachama wa Chadema nchi nzima wapaze sauti zao kumtafuta Mbowe.
“Ikiwa mpaka kufikia kesho Mwenyekiti wetu hatapatikana tutakwenda makamani”- Katibu Mkuu wa CHADEMA John mnyika.
Mbowe na wenzake 11, wamekamatwa ikiwa ni saa chache zilikuwa zimebaki kabla ya kufanyika kwa kingamano la kudai Katiba mpya, mkoani humo.
Kongamano la Kudai Katiba Mpya lililokuwa limepangwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kufanyika Jijini Mwanza limeshindikana mara baada ya viongozi Wakuu wa chama hicho akiwemo Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe kudaiwa kukamatwa usiku wa Manane wakiwa wamelala kwenye Hoteli Walizofikia.
Kongamano hilo lilipangwa kufanyika Jumatano hii Julai 21, 2021 jijini Mwanza ambalo lililenga kuwashirikisha viongozi na wanachama mbalimbali wa chama hicho wakiongozwa na mwenyekiti Freeman Mbowe.
Baadhi ya wakazi wa jijini wa Mwanza ambao walikuwa wakipita katika barabara ya Bwiru wameshuhudia vikosi vya askari Polisi wakiwa wametanda, AQMbapo walotoa mtazamo wao kuiona ni hali ya kutisha na ya kusikitisha katika suala la haki katika demokrasia.
Aidha, Jitihada zilizofanywa na mmoja wa mwandishi wetu katika kumtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Ramadhan Ng’anzi kuzungumzia tukio hilo hazikufanikiwa.