Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imemuachia huru Mdude Nyagali baada ya kutomkuta na hatia katika kesi iliyokuwa ikimkabili ya kusafirisha madawa ya kulevya.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimeandika katika ukurasa wake wa Twitter kuhusu kuachiwa huru kwa mwanaharakati huyo.
Aidha, Hukumu hiyo imefikiwa hii leo Juni 28, 2021 baada ya kuahirishwa tarehe 14 mwezi Juni mwaka huu.
Mwanaharakati Mdude alikuwa akikabiliwa na shtaka la kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroin gramu 23.4 mwaka 2020.
Mwanaharakati huyo pia aliwahi kushtakiwa kwa kosa la uchochezi dhidi ya serikali.