Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega mkaoni Simiyu, limeomba kuanza kusikilizwa kwa kesi za mahakama ya wilaya ndani ya wilaya hiyo ili kuwaondolea usumbufu wananchi wa kusafiri kufuata huduma hiyo mjini Bariadi.
Hatua hii ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, imekuja kufuatia tangu kuanzishwa wilaya hiyo mwaka 2012 mpaka sasa kutokuwa na mahakama ya wilaya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Sundi Mniwe, anaweka msisitizo juu ya jambo hilo, huku Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Busega, Afisa Tarafa ya Busega, David Palangyo akielezea pia.