Star Tv

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema kabla ya kupokea chanjo ya virusi vya Corona ni lazima serikali ijiridhishe kwanza juu ya chanjo hiyo ikiwa ni pamoja na kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa COVID-19.

Rais Samia amesema Ugonjwa wa Covid-19 umeathiri dunia nzima na ili kukabiliana nao lazima kushirikiana na mataifa mengine lakini Serikali itaendelea kuchukua tahadhari mbalimbali ikiwemo matumizi ya chanjo ya ugonjwa huo.

Rais ametoa kauli hiyo leo Mei 14, 2021 katika Baraza la Eid El-Fitir ambalo limefanyika muda wa jioni katika viwanja vya Karimjee mkoani Dar es Salaam.

“Nataka kuhakikishia kwamba tahadhari mlizitoa hapa juu ya chanjo na mengine zitafuatwa kikamilifu na Serikali yenu, hata hivyo hii haina maana kwamba tutapokea kila kitu tunacholetewa au kuambiwa la hasha lazima na sisi tujiridhishe kwa hiyo…tutajiridhisha kabla ya kuamua kutumia au kuacha kutumia, hivyo nawasihi Watanzania kutokuwa na hofu yoyote Serikali ipo makini sana katika kushughulikia suala hilo,” - Amesema Rais Samia.

Aidha, kwa upande wake Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir amewataka Waislamu kuzingatia maagizo yanayotolewa na wataalam wa afya kuhusu kujikinga na maambukizi ya magonjwa mbalimbali ukiwemo Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona.

“Kuna jambo limezungumzwa katika salamu zetu za baraza kuhusu afya. Afya ndio itakayotufanya tuweze kuswali, kufanya ibada, kushughulika masuala ya kiuchumi, kufanya biashara. Uislamu unasema kuilinda afya ni jambo la lazima, tufuate maelekezo ya wataalam wa afya kwa ajili ya kujikinga na magonjwa mbalimbali ikiwemo corona.”-Sheikh Abubakar Zubeir Mufti wa Tanzania

Waumini wa Dini ya Kiislam wameiadhimisha sikukuu hii ya Eid ambapo wametakiwa kuendelea kutenda matendo yaliyo mema kama ambavyo walikuwa wakitenda katika kipindi cha mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.