Star Tv

Mkazi mmoja Wilayani Serengeti aitwaye Happy Nyasumo mwenye umri wa miaka 18 amemuua mumewe, Bebe Mbogo (26) kwa madai kuwa hampendi na hakuwa chaguo lake zikiwa zimepita siku 14 tangu walipofunga ndoa yao.

Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mwanamke aliyefanya kitendo hicho dhidi ya mumewe amekiri kweli kumuua mumewe.

Aidha, Happy amedai kuwa kabla ya yeye kutekeleza mauaji hayo mumewe alimlazimisha kufanya tendo la ndoa na baada ya kumaliza mwanaume alilala na yeye alipobaini amesinzia akachukua panga na kumkata mara tatu shingoni kwasababu hafikirii kama mumewe alikuwa chaguo lake kwa vitendo alivyokuwa akimfanyia.

Aidha mtuhumiwa tayari ameshafikishwa kituo cha polisi ili kuchukuliwa hatua zaidi

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.