Star Tv

Mwili wa hayati Rais Dkt. John Pombe Magufuli utazikwa katika makaburi ya familia huko wilayani Chato, mkoani Geita leo Machi 26,2021.

Maelfu ya Watanzania tayari wameanza kujitokeza katika uwanja wa Magufuli uliopo Chato ambapo misa ya ibada maalumu itafanyika kabla maziko.

Mazishi hayo yataongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi amehudhuri pia, lakini vilevile viongozi wengine wa serikali akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, pamoja na wabunge wa viti maalum akiwemo Ester Matiko na Halima Mdee.

Hayati Rais Dkt. Magufuli ni rais wa kwanza nchini Tanzania kufariki akiwa madarakani na hatua ambayo imeifanya Tanzania kuongozwa na rais mwanamke kwa mara ya kwanza, Rais Samia Suluhu Hassan.

Hayati Rais Dkt. Magufuli alifariki kutokana na maradhi ya moyo wakati alipokuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam Machi 17,2021.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.