Picha mbalimbali za matukio ya msiba wa aliyekuwa Makamu wa kwanza wa rais Zanzibar baada ya kuwasili katika viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo maelfu wamejitokeza kuomboleza msiba huo uliotokea jana Februari 17,2021.
Viongozi mbalimbali ikiwemo marais wastaafu wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein, Abeid Amani Karume na wengine wamehudhuria mazishi ya Maalim Seif Sharif Hamad
Kisiwani Pemba ambapo ndio ilikuwa ngome yake Kuu wakati wa uhai wake, punde tu baada ya taarifa za kifo chake kuenea hapo jana, baadhi ya maduka yamefungwa na shughuli nyingi za mji kusimama, hivyo kufanya mji huo kuzizima kwa saa kadhaa.
Ratiba ya mazishi inaonyesha kuwa, mwili wa marehemu utakwenda kupumzishwa kijijini kwao Mtambwe-Pemba.
#RIPMaalimSeifSharifHamad