Star Tv

Makamu wa Kwanza wa Rais visiwani Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amefariki dunia.

Habari hizo zimethibitishwa leo na Rais wa Zanzibar, Dokta Hussein Ali Hussein Mwinyi wakati akizungumza na waandishi wa habari visiwani humo.

Rais Dkt. Mwinyi amesema Maalim amefariki Dunia majira ya saa tano asubuhi leo Februari 17,2021.

Amesema Makamu huyo wa Rais amefariki katika hospitali ya Muhimbili ambapo alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu tangu Februari 09,2021.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa pole pamoja na salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, Watanzania, pamoja na Chama cha ACT Wazalendo kufuatia msiba huo.

Aidha, Rais Mwinyi ametangaza siku saba za maombolezo ambapo amesema bendera zitapepea nusu mlingoti, Na kusema taarifa zaidi za msiba huo zitaendelea kutolewa kadiri itakavyowezekana kupitia serikali kwa kushirikiana na familia yake pamoja na Chama cha ACT Wazalendo.

Maalim Seif Sharif amefariki dunia akiwa ametumikia wadhifa wa makamu wa kwanza wa rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa chini ya siku 100, akiwa sehemu ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyoundwa baada ya Uchaguzi Mkuu 2020.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.