Star Tv

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, ameitaka Bodi ya mfuko wa Barabara (RfB) kutumia vifungu vya sheria vitakavyowabana watumiaji wa barabara wanaoegesha magari kwenye mabega ya barabara, wanaoiba alama za barabarani pamoja na wanaopitisha mifugo kwenye barabara.

Mhandisi Kasekenya ameyasema hayo, alipotembelea ofisi za Mfuko huo zilizoko Njedengwa, jijini Dodoma ili kujifunza shughuli zinazofanywa na mfuko huo.

“Simamieni sheria na muwachukulie hatua wale wote wanaohujumu miundombinu ya barabara kwa namna moja ama nyingine ili tuzilinde barabara zetu na kutotumia fedha nyingi katika matengenezo”. amesema Mhandisi Kasekenya.

Aidha, amewataka Mameneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) na wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kuhakikisha wanaziba mashimo barabarani ndani ya masaa 48 kama sheria inavyoelekeza ili kupunguza ajali zinazoweza kutokea kutokana na uwepo wa mashimo hayo.

Meneja wa Bodi ya Mfuko wa Barabara Eliud Nyauhenga, pamoja na mambo mengine amemueleza Naibu Waziri huyo kuwa Mfuko unafanya shughuli mbalimbali ikiwemo kukusanya fedha, kugawa fedha kwa Taasisi husika pamoja na kufuatilia matumizi ya fedha hizo.

Nyauhenga amebainisha kuwa asilimia 70 ya makusanyo inapelekwa kwenye ukarabati wa barabara za kitaifa ambazo ziko chini ya wakala wa Barabara nchini (TANROADS) na asilimia 30 inapelekwa kwenye ukarabati wa barabara zilizoko chini ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA).

Naibu Waziri Kasekenya, ametembelea Bodi ya Mfuko wa Barabara ambayo imekuwa ikitoa fedha kwa ajii ya matengenezo ya barabara nchini zinazosimamiwa na TANROADS pamoja na TARURA na kuhakikisha kuwa hali ya mtandao wa barabara nchini inakuwa bora.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.