Star Tv

Kundi la Islamic State (IS), kupitia shirika lake la propaganda AMAQ, limekiri kuhusika na shambulio lililogharimu maisha ya afisa mmoja wa kikosi cha ulinzi wa taifa jana Jumapili huko Sousse, mji wa kitalii Mashariki mwa Tunisia.

Jumapili mapema asubuhi, watu waliokuwa kwenye gari waliwavizia maafisa wa kikosi cha ulinzi wa taifa karibu na eneo lililo karibu na bandari ya Kantaoui, katika mji wa kitalii wa Sousse, kisha wakawashambulia kwa kisu, na kumuua mmoja wao na pia kumjeruhi vibaya mwingine.

Kundi la IS limetangaza kifo cha afisa mmoja wa vikosi vya usalama katika shambulio lililofanywa na "wapiganaji" wa kundi hilo, bila hata kutoa maelezo zaidi.

Wauaji watatu, ikiwa ni pamoja na ndugu wawili, waliuawa Jumapili asubuhi katika eneo hilo hilo na hawakuwa wanajulikana na mamlaka nchini Tunisia.

Watu saba pia walikamatwa kuhusiana na uchunguzi huo, ikiwa ni pamoja na mke wa mmoja wa washambuliaji, ndugu wawili na mtu mmoja anayeshukiwa kuwa msajili, kimebaini kikosi cha ulinzi wa taifa.

Shambulio hili jipya dhidi ya vikosi vya usalama, katika jiji ambalo moja ya mashambulizi mabaya ya kijihadi ambayo yaliikumba nchi hiyo mwaka 2015, lilitokea siku tatu baada ya serikali mpya kuapishwa, baada ya mvutano mkali wa kisiasa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.