Star Tv

Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kwamba "janga la Corona linaongezeka kwa kasi" na kukiri kwamba "ushahidi unaonyesha" kuwa kuna uwezekano virusi vya Corona kusambazwa kwa njia ya hewa.

Kauli hiyo inakuja baada ya kundi la wanasayansi 239 wa kimataifa kutoa tahadhari kuhusu njia hii ya maambukizi.

Zaidi ya wanasayansi 200 wa kimataifa wameitaka WHO na jamii ya kimataifa ya matibabu "kutambua uwezekano wa maambukizi ya virusi vya Corona kwa njia ya hewa," katika barua ya wazi iliyochapishwa Jumatatu katikaGazeti la Magonjwa ya Kuambukiza, Clinical Infectious Diseases, ya huko Oxford.

Hoja ambayo Shirika la Afya Duniani linapaswa kuchunguza, kwa mujibu wa Isabella Annesi-Maesano, moja wa wanasayansi hao waliotia sani kwenye barua hiyo. Ni mkurugenzi wa utafiti katika Inserm, mtaalam wa magonjwa ya kuambukia na magonjwa ya kupumua.

Shirika la Afya Duniani linasema hakuna ushahidi, lakini nataka kusema kwamba kukosekana kwa ushahidi sio dhibitisho la kutokuwepo. Nina maanisha kwamba kuna data nyingi na hata ikiwa hakuna data kama hiyo WHO wanapaswa kuwa waangalifu, Profesa Isabella Annesi-Maesano, amesema katika mahojiano na Valérie Cohen.

"Tunatambua kuwepo na ushahidi na tunapaswa tuwe wazi kwa uwezekano huu na kuelewa athari zake," amesema Benedetta Allegranzi, afisa wa WHO, katika mkutano na waandishi wa habari.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.