Star Tv

Miaka saba iliyopita Amol Yadav alitangaza kwa familia yake na marafiki kuwa angejenga ndege kwenye paa la nyumba yao katika mji wa Mumbai India.

Familia na marafiki waliokua wamepigwa na butwa walimuuliza rubani huyo ni vipi angeweza kuishukisha ndege ikikamilika . Walijikakamua kupandisha vifaa vya kuijengea ndege hiyo hadi paa la nyumba ya familia la ghorofa tano, ikiwemo injini iliyonunuliwa kutoka ng'ambo ya zaidi ya kilo 180.

Mwezi Februari mwaka uliopita, ndege hiyo ya injini moja yenye nafasi ya watu 6 ilikuwa imekamilika.

Kulingana na Bwa Yadavm, ndege hiyo ndiyo ya kwanza kujengewa nyumbani nchini India.

Anasema kuwa injini hiyo ina nguvu za kuiwezesha ndege hiyo kupaa umbali wa futi 13,000 na tanki lake linaweza kubeba mafuta ya kuiwezesha ndege hiyo kusafiri umbali wa kilomita 2000 kwa kasi ya kilomita 342 kwa saa.

Bwana Yadav sasa anasema kuwa yuko tayari kujenga ndege ya kwanza kabisa kujengwa India.

Wawekezaji wameonyesha moyo wa kuwekeza na serikali ya BJP imeahidi kumpa ekari 157 za ardhi za kujenga kiwanda cha kuunda ndege za kubeba abiria 19.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.