Mapigano ‘makali’ kati ya wanajeshi wa Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo na wasi wa M23 katika eneo la Rutshuru yameendelea kwa siku ya sita ambapo imethibitishwa kuwa eneo la Ntamugenga limetekwa na M23.
Jumapili mapigano yalifanyika katika mji mdogo wa Ntamugenga uliopo umbali wa kilomita 15 kutoka Rutshuru.
Hapo jana Jumatatu, vyombo vya habari vya DRC vilimnukuu Msemaji wa jeshi ya Congo Luteni Jenerali Guillaume Njike Kaiko akithibitisha kuwa eneo hilo limetekwa na wapiganaji wa M23.
#ChanzoBBC