Star Tv

Rishi Sunak sasa atachukua nafasi ya Waziri Mkuu katika wakati mgumu sana kwa uchumi wa taifa hilo, Ambapo bado haijasikika mipango yoyote ya kina kutoka kwake tangu kampeni ya uongozi katika msimu wa joto.

Rishi Sunak amepanda jukwaani kwa hotuba yake ya kwanza kwa umma kama kiongozi wa Tory ambapo ametoa pongezi kwa Liz Truss kwa uongozi wake "wenye heshima" "chini ya hali ngumu nje ya nchi na nyumbani".

Sunak ameahidi kutumikia kwa uadilifu na unyenyekevu nafasi hiyo ya Uwaziri Mkuu, "nitafanya kazi siku baada ya siku kwa ajili ya watu wa Uingereza. Ninaahidi kuwa nitahudumu kwa uadilifu na unyenyekevu," Sunak alisema.

Rishi Sunak amesema Uingereza ni nchi kubwa lakini inakabiliwa na changamoto "kubwa" za kiuchumi.

Wiki saba baada ya kushindwa katika uchaguzi wa viongozi wa Conservative, Rishi Sunak sasa atakabidhiwa ufunguo wa Downing Street.

Sunak ni Waziri Mkuu wa kwanza wa Uingereza mwenye asili ya Asia, na atachukua madaraka huku Uingereza ikikabiliwa na changamoto kubwa za kiuchumi.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.