Star Tv

Maelfu ya waandamanaji wamejitokeza katika mitaa ya mji mkuu wa Tunisia kuandamana dhidi ya Rais wa nchi hiyo.

Maandamano kama hayo ya makundi ya kisiasa yanayopingana vikali yalifanyika mjini Tunis.

Makundi yote mawili yalimkashifu Rais Kais Saied kwa kuwa mbabe ambaye anabadilisha na kufifisha maendeleo ya kidemokrasia yaliyopatikana tangu ghasia za 2011.

Aidha pia waandamanaji hao walitaka uwajibikaji kutokana na mdodoro wa kiuchumi nchini humo ambao umeshuhudia uhaba mkubwa wa chakula na mafuta.

Wakosoaji wa Rais Saied wanamtuhumu kwa kufanya mapinduzi na kujaribu kurudisha Tunisia katika utawala wa kiimla mfumo wa serikali unaoendeshwa na mtu mmoja mwenye mamlaka kamili.

#ChanzoBBC

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.