Star Tv

Waziri Mkuu wa Uingereza Liz Truss amemfuta kazi waziri wake wa fedha, Kwasi Kwarteng, muda mfupi kabla ya kiongozi huyo kupanga kuachana na hatua za kiuchumi katika jitihada za kujinusuru na misukosuko ya kisiasa inayoikabili nchi hiyo.

Truss, aliye madarakani kwa siku 37 pekee, anatathmini upya hatua za punguzo la ushuru zilizosababisha ongezeko la gharama za ukopaji na kuilazimu Benki Kuu ya Uingereza kuingilia kati.

Aidha aliyekuwa waziri wa mambo ya nje, Jeremy Hunt, ameteuliwa kuwa waziri mpya wa fedha kujaza nafasi ya Kwarteng.

Bado haijafahamika ni vipi kufutwa kazi kwa waziri huyo wa fedha kunaweza kumnusuru Truss na shinikizo kubwa dhidi yake, akilaumiwa kuwa kigeugeu kwenye utawala wake.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.