Rais wa Marekani Joe Biden amesema hatua ya Rais wa Urusi Vladimir Putin la kutumia silaha za nyuklia linatishia kuleta hatari kubwa kama hiyo tangu Mgogoro wa Kombora la Cuba, akiongeza kuwa Washington ilikuwa "inajaribu kubaini" njia ya Putin ya kujiondoa.
Ikulu ya White House imesema mara kwa mara kwamba haijaona dalili zozote kwamba Urusi inajiandaa kutumia silaha za nyuklia licha ya kile inachokiita "ugomvi wa nyuklia" wa Putin.
Rais Biden siku ya Alhamisi aliweka wazi kuwa alikuwa "akimwangalia Putin na jinsi anavyoweza kujibu wakati jeshi la Ukraine likipata mafanikio dhidi ya uvamizi wake".
"Kwa mara ya kwanza tangu Mgogoro wa Kombora la Cuba, tuna tishio la moja kwa moja kwa matumizi ya silaha za nyuklia, ikiwa mambo yataendelea kama yalivyokuwa,"-Rais Biden.
Aidha Biden amebainisha kwamba yeye na maafisa wa Marekani wanatafuta njia ya kidiplomasia. "Tunajaribu kufahamu ni nini njia panda ya Putin...anapata wapi njia ya kutoka? sio tu kupoteza heshima lakini kupoteza nguvu kubwa nchini Urusi,"- Biden.
#ChanzoBBC