Star Tv

Rais wa Marekani Joe Biden amesema hatua ya Rais wa Urusi Vladimir Putin la kutumia silaha za nyuklia linatishia kuleta hatari kubwa kama hiyo tangu Mgogoro wa Kombora la Cuba, akiongeza kuwa Washington ilikuwa "inajaribu kubaini" njia ya Putin ya kujiondoa.

Ikulu ya White House imesema mara kwa mara kwamba haijaona dalili zozote kwamba Urusi inajiandaa kutumia silaha za nyuklia licha ya kile inachokiita "ugomvi wa nyuklia" wa Putin.
Rais Biden siku ya Alhamisi aliweka wazi kuwa alikuwa "akimwangalia Putin na jinsi anavyoweza kujibu wakati jeshi la Ukraine likipata mafanikio dhidi ya uvamizi wake".

"Kwa mara ya kwanza tangu Mgogoro wa Kombora la Cuba, tuna tishio la moja kwa moja kwa matumizi ya silaha za nyuklia, ikiwa mambo yataendelea kama yalivyokuwa,"-Rais Biden.

Aidha Biden amebainisha kwamba yeye na maafisa wa Marekani wanatafuta njia ya kidiplomasia. "Tunajaribu kufahamu ni nini njia panda ya Putin...anapata wapi njia ya kutoka? sio tu kupoteza heshima lakini kupoteza nguvu kubwa nchini Urusi,"- Biden.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.