Star Tv

Kiongozi mkuu wa Iran amezilaumu Marekani na Israel kwa kuchochea maandamano yaliyoenea nchini humo kufuatia kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa chini ya ulinzi wa polisi.

Katika tamko lake la kwanza hadharani kuhusu machafuko hayo, Ayatollah Ali Khamenei amesema "machafuko" yalikuwa "yamepangwa" na maadui wakubwa wa Iran na washirika wao.

Maandamano hayo ni changamoto kubwa kwa utawala wake kwa muongo mmoja, na alivitaka vikosi vya usalama kuwa tayari kwa zaidi.

Marekani imesema "imeshtushwa" na majibu ya vurugu kwa maandamano hayo.

Rais Joe Biden amesema "ana wasiwasi mkubwa" kuhusu ripoti za "kuongezeka kwa ukandamizaji wa vurugu dhidi ya waandamanaji wa amani".

Biden amesema Waandamanaji hao walikuwa wakitoa wito wa "kanuni za haki na za ulimwengu wote, "inasimama na wanawake wa Iran" ambao walikuwa "wakiuhamasisha ulimwengu kwa ushujaa wao".

Uingereza iliunga mkono kauli hizo, ikitoa wito kwa mwanadiplomasia mkuu wa Iran mjini London kuwaambia viongozi wao mjini Tehran kwamba "badala ya kuwalaumu wahusika wa nje kwa machafuko hayo, wanapaswa kuwajibika kwa matendo yao na kusikiliza kilio cha watu wao".

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.