Star Tv

Polisi wa Urusi wameripotiwa kuwakamata mamia ya waandamanaji waliokuwa wakiandamana kupinga uamuzi wa Urusi wa kuongeza maelfu ya wanajeshi wa ziada kupigana nchini Ukraine.

Kikundi cha haki za binadamu cha Urusi OVD-Info kiliweka jumla ya idadi ya waliokamatwa kuwa zaidi ya 1,300.

Idadi kubwa zaidi ya waliokamatwa walikuwa raia wa St. Petersburg na Moscow.

Nchini Urusi, mikutano isiyoidhinishwa ni kinyume cha sheria chini ya sheria za kupinga maandamano.

Jana, ofisi ya mwendesha mashitaka ya Moscow ilionya kwamba wito kwenye mtandao wa kujiunga na maandamano yasiyoidhinishwa ya mitaani, au kushiriki katika maandamano hayo, inaweza kusababisha mwananchi kufungwa jela kwa miaka 15.

#ChanzoBBC

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.