Star Tv

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema maafisa wa Umoja wa Mataifa watapewa kibali cha kuzuru na kukagua kinu na kambi ya nyuklia ya Zaporizhzhia.

Ikulu ya Kremlin imetoa tangazo hilo baada ya mazungumzo kwa njia ya simu kati ya Putin na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.

Hatua hiyo inakuja huku madai ya mapigano karibu na mtambo huo yakiendelea, na kusababisha raia wanne kujeruhiwa na makombora ya Urusi.

Mbali na hilo, Marekani hapo jana siku ya Ijumaa imeahidi kutuma silaha na risasi zaidi kusaidia katika juhudi za vita vya Ukraine.

Kufuatia mazungumzo ya viongozi hao wa Ufaransa na Urusi, Kremlin ilisema, Putin amekubali kuwapa wachunguzi wa Umoja wa Mataifa "msaada unaohitajika" ili kufikia eneo la nyuklia la Zaporizhzhia.

Kinu hicho kimekuwa chini ya umiliki wa Warusi tangu mapema Machi lakini mafundi wa Kiukreni bado wanakiendesha chini ya maelekezo ya Urusi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.