Star Tv

Mwanasheria mkuu wa zamani wa Mexico amekamatwa akihusishwa na kutoweka kwa wanafunzi 43 mwaka wa 2014.

Jesús Murillo Karam, ambaye aliongoza uchunguzi wa ukatili huo, ameshtakiwa kwa kutoweka kwa wanafunzi hao, mateso na kuzuia haki kutendeka.

Wanafunzi hao walitoweka walipokuwa wakisafiri kwa basi kupitia mji wa Iguala wakielekea kwenye maandamano katika Jiji la Mexico.

Zaidi ya vipande vya mifupa vichache vilivyopatikana kutoka kwa watatu kati yao 43, hakuna kilichoonekana wala kujulikana juu ya hatima yao.

Inaelezwa Polisi walifyatulia risasi mabasi yaliyokuwa yamewabeba wanafunzi jioni ya tarehe 26 Septemba 2014 lakini kilichotokea baadaye kimeibua mjadala.

Kutoweka kwao kwa kushangaza kulileta mshtuko kote ulimwenguni na kusababisha maandamano makubwa nchini Mexico dhidi ya vitendo vya kutokujali na kushiriki katika uhalifu.

Siku ya Alhamisi, tume iliyoundwa na Rais wa sasa Andrés Manuel López Obrador ilishutumu wanajeshi kwa kuhusika na mauaji hayo, japokuwa sio moja kwa moja bali angalau kwa uzembe.

Mapema mwaka huu Rais López Obrador alifichua kuwa wanajeshi wa wanamaji walikuwa wakichunguzwa kwa madai ya kuvuruga ushahidi, ikiwa ni pamoja na katika eneo la kutupa taka ambapo mabaki ya binadamu yalipatikana.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.