Waziri mkuu wa Uingereza amesema kufanya mazungumzo na Urusi ili kumaliza vita huenda suala hilo lisiwezekane.
Boris Johnson amenukuliwa akisema "kushughulika na Rais Putin wa Urusi ni sawa na kujadiliana na mamba akiwa ameweka mguu wako kwenye taya zake".
Akizungumza na waandishi wa habari akiwa kwenye ndege kuelekea India, Waziri Mkuu wa Uingereza amesema Putin anaweza tu kukubali mazungumzo ikiwa atapata nafasi ya kuongeza nguvu zake nchini Ukraine.
Boris ameonya kuwa kiongozi huyo wa Urusi anaweza kutafuta kuanzisha mashambulizi mapya katika mji mkuu wa Kyiv huko nchini Ukraine.