Star Tv

Benki ya Dunia imesema inatarajia uchumi wa Ukraine utapungua kwa 45% mwaka huu kutokana na vita.

Benki hiyo imetabiri pia kuwa kutakuwa na uharibifu mkubwa wa kiuchumi kuliko uliosababishwa na janga la Covid-19 kote Ulaya mashariki na Asia ya kati, na vikwazo ambavyo havijawahi kushuhudiwa na kusababisha mdororo mkubwa wa uchumi nchini Urusi pia.

Sehemu kubwa ya wafanyakazi wa Ukraine wamelazimika kukimbia na biashara nyingi zimefungwa, huku barabara, viwanda na miundombinu mingine ikiharibiwa.

Benki ya Dunia imebainisha pia juu ya maendeleo ya miaka mingi ya nchi hiyo ikisema yamebatilishwa. "Ukraine ilikuwa chanzo kikuu cha mazao kama vile alizeti na ngano lakini kutokana na mauzo ya nje kusitishwa bei ya vyakula duniani imepanda".

Vikwazo dhidi ya Urusi vinamaanisha kuwa benki ya Dunia inatabiri uchumi wake kupungua zaidi ya 11% mwaka huu.

#ChanzoBBC

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.