Star Tv

Ukraine imekataa kusalimisha Mariupol, ikikataa ombi la Urusi la kuacha jiji hilo kufikia makataa ya saa 05:00 saa za Moscow (02:00 GMT)

Urusi ilikuwa imejitolea kuweka korido za kibinadamu ili wakazi waweze kuondoka jiji hilo

Takriban watu 300,000 wamenaswa na chakula kidogo, maji na umeme katika jiji hilo ambalo limekuwa likilipuliwa kwa bomu kwa muda wa wiki mbili zilizopita.

Urusi imeshambulia makazi kadhaa ya raia, shule, hospitali na ukumbi wa michezo. Ukraine imesema mashambulizi ya Mariupol ni uhalifu wa kivita ambao utaingia katika historia

Kulikuwa na utulivu wa saa 24 katika kupiga makombora katika miji mingi siku ya Jumapili. Lakini huko Kyiv, mji mkuu ulishuhudia mashambulizi ambayo yaliua watu wanne.

Rais wa Ukraine Zelensky pia ameikosoa Israel kwa kusitasita kutuma teknolojia yake ya ulinzi wa makombora nchini Ukraine.

Katika hotuba yake kwa bunge la Israel, alisema: “Kila mtu anajua mifumo yenu ya ulinzi ya makombora ndiyo bora zaidi… bila shaka mnaweza kuwasaidia watu wetu.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.