Star Tv

Takriban watu 22 wafariki kufikia sasa baada ya matetemeko ya ardhi ya mfululizo kukumba magharibi mwa Afghanistan siku ya Jumatatu, maafisa walisema.

Kwa mujibu wa data kutoka Shirika la Jiolojia la Marekani (USGS), matetemeko hayo ya kipimo cha 4.9 na 5.3 yaliathiri mkoa wa kaskazini-magharibi wa Badghis, ambako na kusababisha nyumba na majengo kuporomoka.

Msemaji ameliambia shirika la habari la AFP kuwa watoto wanne ni miongoni mwa waliopatikana wamekufa kwenye vifusi.

Matetemeko ya ardhi yanaweza kusababisha uharibifu mkubwa nchini Afghanistan, ambapo makao mengi hayajaimarishwa au hayajajengwa vizuri.

USGS ilinakili matetemeko mawili ya ardhi siku ya Jumatatu, ambayo yalipiga takriban kilomita 50 (31mi) kutoka Qala-e-Naw, mji mkuu wa jimbo hilo.

Tetemeko la kwanza lilipiga alasiri, na la pili likafuata saa mbili baadaye. Athari zake zilionekana zaidi katika wilaya za Qadis na Mugr.

#ChanzoBBC

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.