Star Tv

Kiongozi wa Kazakhstan anayeiongoza nchi hiyo kimabnavu anasema ameidhinisha vikosi vya usalama "kufyatua risasi bila onyo" huku kukiwa na msako mkali dhidi ya maandamano dhidi ya serikali.

Rais Kassym-Jomart Tokayev pia alisema "majambazi 20,000" wameshambulia mji mkuu wa Almaty, kitovu cha maandamano yaliyochochewa na ongezeko la bei ya mafuta.

Wizara ya mambo ya ndani inasema "wahalifu wenye silaha" 26 na maafisa wa usalama 18 wameuawa kufikia sasa katika machafuko hayo.

Katika hotuba yake kwa njia ya televisheni, Bw Tokayev alisema vikosi vya kulinda amani vilivyotumwa kutoka Urusi na mataifa jirani vimefika kwa ombi lake na viko nchini kwa muda ili kuhakikisha usalama.

Kikosi kutoka kwa Jumuiya ya Mkataba wa Usalama wa Pamoja (CSTO) inayoongozwa na Urusi inaripotiwa kuwa na wanajeshi 2,500. Bw Tokayev alitoa "shukrani maalum" kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin kwa kutuma wanajeshi.

Mapema siku ya Ijumaa, milio mipya ya risasi ilisikika karibu na uwanja mkuu wa Almaty.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.