Mwanzilishi wa mtandao wa wikileaks Julian Assange ameruhusiwa kufunga ndoa akiwa jela.
Julian Assange amepatiwa ruhusa ya kumuoa mpenzi wake Stella Moris katika jela ya Belmarsh.
Mwanzilishi huyo wa mtandao wa Wikileaks na Bi. Moris wana watoto wawili wa kiume, ambao alisema walipatikana wakati alipokuwa akiishi katika ubalozi wa Ecuador mjini London.
Huduma ya jela hiyo imesema kwamba ombi la Assange liliruhusiwa na gavana wa jela hiyo.
Wafungwa wana haki ya kuomba kufunga ndoa wakiwa jela chini ya kifungu cha ndoa cha 1983 na ombi hilo linaporuhusiwa wanapaswa kusimamia gharama zote za ndoa hiyo bila usaidizi wowote wa fedha za umma.
Katika mahojiano na gazeti la Mail la siku ya Jumapili mwaka uliopita, Bi Moris ambaye ni wakili wa Afrika Kusini, alifichua kwamba alikuwa katika uhusiano na Assange tangu 2015 na amekuwa akiwalea watoto wao wawili yeye binafsi.