Star Tv

Mwanzilishi wa mtandao wa wikileaks Julian Assange ameruhusiwa kufunga ndoa akiwa jela.

Julian Assange amepatiwa ruhusa ya kumuoa mpenzi wake Stella Moris katika jela ya Belmarsh.

Mwanzilishi huyo wa mtandao wa Wikileaks na Bi. Moris wana watoto wawili wa kiume, ambao alisema walipatikana wakati alipokuwa akiishi katika ubalozi wa Ecuador mjini London.

Huduma ya jela hiyo imesema kwamba ombi la Assange liliruhusiwa na gavana wa jela hiyo.

Wafungwa wana haki ya kuomba kufunga ndoa wakiwa jela chini ya kifungu cha ndoa cha 1983 na ombi hilo linaporuhusiwa wanapaswa kusimamia gharama zote za ndoa hiyo bila usaidizi wowote wa fedha za umma.

Katika mahojiano na gazeti la Mail la siku ya Jumapili mwaka uliopita, Bi Moris ambaye ni wakili wa Afrika Kusini, alifichua kwamba alikuwa katika uhusiano na Assange tangu 2015 na amekuwa akiwalea watoto wao wawili yeye binafsi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.