Star Tv

Mamia ya watu wamejitoalea kuvua nguo zao na kubaki watupu ili wachorwe picha zinazoelezea namna Bahari ya kifo au 'Dead Sea' inavyoendelea kunyauuka.

Watu hao wake kwa waume wapatao 300, walikuwa wamevaa nguo za ndani nyeupe na hivyo kuacha sehemu nyingine za mwili wao wazi ili kutoa fursa kwa mpiga picha Mmarekani Spencer Tunick, ambaye amefanya sanaa hiyo katika maeneo mengine ya fukwe za bahari duniani kama njia ya kuhamasisha watu kutunza bahari.

Mpiga picha huyo amewahi kuendesha kampeni hiyo katika maeneo kama eneo la barafu la Uswiss na ufukwe wa Afrika Kusini.

“Matembezi yangu nchini Israeli yamenipa uzoefu wa kipekee na ninafurahi wakati wote kurejea hapa na kupiga picha katika nchi pekee ya Mashariki ya Kati inayoruhusu sanaa ya aina hii,”- Alisema Tunick.

Aidha inaelezwa kuwa upigaji picha huo ulihamasishwa na Wizara ya utalii ya Israeli.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.