Star Tv

Marekani imetoa taarifa ya kulaani vikali mapinduzi yaliyotokea Guinea, Ambapo imetoa taarifa hiyo imevitaka vyama vya siasa kuacha ghasia na kufuata sheria.

Marekani imesema kuwa ghasia na hatua zozote zile zilizopo nje ya katiba zitaathiri ustawi wa Guinea, amani na utulivu.

Aidha wamesisitiza kuwa midahalo ya kitaifa inapaswa kuwa ya wazi na inayolenga kupata suluhu ya demokrasia na amani.

Taarifa hiyo imekuja na taarifa nyingine za kimataifa kukemea kupinduliwa kwa rais Alpha Condé.

Jumuiya ya kiuchumi ya Afrika Magharibi, Ecowas, ililaani "jaribio la mapinduzi" na ikathibitisha "kutokubali mabadiliko yoyote ya kisiasa yanayopingana na katiba".

Imetaka rais Condé aheshimiwe na wale wote waliokamatwa pamoja naye waachiwe huru.

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na Umoja wa Afrika tayari wameshutumu mapinduzi hayo na kutaka Rais Condé aachiwe huru.

Hatima ya rais huyo bado haijawekwa wazi baada ya video ambayo haijathibitishwa kuonesha Rais akiwa amezungukwa na askari ambao wanadai wamechukua mamlaka ya nchi.

Hata hivyo wizara ya usalama ilisema jaribio hilo la mapinduzi, liliweza kuzuiwa na walinzi wa rais.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.