Star Tv

Mashambulizi ya Marekani ya ndege zisizo na rubani katika mji mkuu Kabul umezuia shambulio jingine baya la kujitoa uhanga katika uwanja wa ndege, maafisa wa jeshi la Marekani wamesema.

Shambulio hilo lililenga gari lililobeba takribani mtu mmoja anayehusishwa na kundi la Islamic State, tawi la Afghanistan, jeshi la Marekani limeeleza.

Marekani ilionya juu ya uwezekano wa mashambulio mengine wakati operesheni za kuondoa raia zikitamatika.

Pamoja na hayo, imesema kuwa itaendelea kuwaondoa Waafghan kutoka uwanja wa ndege wa Kabul hadi "saa za mwisho".

Tarehe ya mwisho ya ujumbe wa uokoaji ya Agosti 31 ilikubaliwa kati ya Marekani na Taliban, ambao sasa wanadhibiti sehemu kubwa ya nchi.

Ndege za mwisho zinazowarudisha wanajeshi wa Uingereza kutoka Afghanistan zimekuwa zikiwasili nchini Uingereza siku ya Jumapili.

Marekani inasema imewezesha uokoaji wa watu zaidi ya 110,000 kutoka uwanja wa ndege wa Kabul tangu tarehe 14 mwezi Agosti - siku moja kabla ya Taliban kuchukua udhibiti wa mji mkuu.

Wengi wao wanahisi hawawezi kuwa na mustakabali waliojiandaa nao baada ya miongo miwili ya ushiriki wa kimataifa, mwandishi wetu anasema - na wengi wanasema Taliban wanawazuia kuondoka.

Siku ya Jumapili, Kapteni Bill Urban alisema Marekani ilifanya mashambulizi lililolenga "kuondoa tishio karibu" na uwanja wa ndege wa Kabul.

"Tuna imani tumefanikiwa kufikia lengo," alisema, na kuongeza: "Milipuko ya pili kutoka kwenye gari ilionesha uwepo wa idadi kubwa ya vifaa vya kulipuka."

Maoni yake yalikuja baada ya ripoti nyingi za mlipuko mkubwa uliosikika karibu na uwanja wa ndege wa Kabul. Picha nyigine zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii zilionesha mawingu meusi ya moshi yanayopanda hewani juu ya majengo.

Maafisa wa ujasusi wa Marekani mapema walisema wamepokea vitisho '', vya kuaminika" dhidi ya uwanja wa ndege, na kwamba wanajeshi wataendelea kutekeleza mashambulizi pale inapobidi.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.