Mwandishi na Mpiga picha wa gazeti la Times Marcus Yam, amekuwa akisimulia tukio aliloshuhudia karibu na uwanja wa ndege wa Kabul siku ya Jumanne.
Yam amesema alishuhudia makumi ya watu wa Taliban wakipiga risasi hewani, na silaha zao zikilenga umati wa watu. Aidha walitumia vitu kama vile fimbo, kamba na njia zingine kuwapiga raia.
Picha za ugofya zilizonaswa zinaonyesha mwanamke mmoja aliumizwa na mtoto mdogo akaachwa akiwa anatoka damu kutokana na kile kinachoonekana kuwa jeraha la kichwa.
Yam pia aliandika kwamba yeye mwenyewe alichapwa mguuni wakati anapiga picha matukio yanayoendelea eneo hilo.