Star Tv

Rais wa Belarus Alexander Lukashenko amezituhumu nchi za Magharibi kwa kujaribu kutumia tukio la kulazimishwa kutua mjini Minsk ndege ya Ryanair mwishoni mwa wiki ili kuanzisha vita vya kisiasa dhidi yake na kusema zimetumia uwongo kueleza jinsi alivyolishughulikia tukio hilo.

Katika matamshi yake ya kwanza baada ya baadhi ya wanasiasa wa Ulaya kuliita tukio hilo la Jumapili kuwa ni "utekaji nyara uliofadhiliwa na serikali", Lukashenko ameliambia bunge kuwa alichukua hatua halali na kwa mujibu wa sheria zote za kimataifa, lakini watu wenye nia mbaya wanajaribu kutumia tukio hilo la ndege kuhujumu utawala wake. Belarus ilitumia kisa hicho kumkamata mwandishi wa habari wa siasa za upinzani aliyekuwemo ndani ya ndege hiyo Raman Pratasevich. Kiongozi wa upinzani aliyeko uhamishoni Sviatlana Tsikhanouvskaya amesema leo kuwa upinzani unajiandaa kwa awamu mpya ya maandamano ya kuipinga serikali nchini Belarus.

CHANZO:

IDHAA YA KISWAHILI (DW)

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.