Star Tv

Mji Mkuu wa Somalia Mogadishu, Jumatatu hii umeripotiwa kuwa shwari baada ya mapigano kati ya wanaounga mkono upinzani na vikosi vya usalama vya serikali, Redio binafsi ya Risala imeripoti.

Mapigano makali kati ya wapiganaji watiifu wa upinzani na vikosi vya usalama vya serikali yalizuka siku ya Jumapili.

''Hali katika maeneo yaliyotokea mapigano yamekuwa shwari hii leo na watu walionekana wakitembea katika maeneo yao ya kazi na wengine walitoka kwa ajili ya kutathimini hali ilivyo'' -tovuti ya Redio ya Risala imeeleza.

Mapigano yamezuka katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu kati ya makundi kinzani ya vikosi vya usalama nchini humo.

Ripoti zinasema kwamba silaha kali zilitumika huku makombora yakirushwa karibu na kasri la rais.

Baadhi ya vikosi hivyo vinamuunga rais Mohammed Abdaullahi Mohammed huku vingine vikimpinga.

Wiki iliyopita bwana Mohammed anayejulikana kama Farmajo kwa utata alijiongezea muda wake ofisini, Muhula wake uliisha rasmi mwezi Februari.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.