Star Tv

Mtu mmoja amepigwa risasi na kufariki baada ya kuliendesha gari lake kuelekea kwa maafisa wawili wa polisi karibu na majengo ya bunge nchini Marekani, Ambaye pia amesababisha kifo cha Afisa wa polisi mmoja.

Maafisa wa polisi wamesema gari hilo lililokuwa likiendeshwa kuelekea walipo maafisa wa polisi liligonga vizuizi vya usalama, kisha mshukiwa aliyekuwa akiliendesha akatoka nje akiwa amebeba kisu mkononi na kukimbia kuelekea kwa maafisa wa polisi.

Aidha, imeelezwa kuwa fisa mmoja wa polisi amekufa kufuatia kisa hicho.

Mtuhumiwa wa shambulizi hilo inaelezwa kuwa, aliliendesha gari kuelekea kwa maafisa hao wawili waliokuwa wakishika doria katika majengo ya bunge ya Marekani mjini Washington DC, kabla ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi.

Mshukiwa huyo alikaidi amri kutoka kwa maafisa wa usalama na ndipo alipopigwa risasi, na katika harakati za kumpeleka kupata matibabu baadaye alifariki akiwa hospitalini.

Rais wa Marekani Joe Biden ambaye hayuko mjini Washington kwa sasa amesema yeye pamoja na mke wake Jill Biden wamesikitishwa na shambulizi hilo.

"Jill pamoja na mimi tulisikitishwa kusikia kuhusu shambulizi katika eneo la kizuizi cha usalama kwenye majengo ya bunge ambalo limesababisha kifo cha afisa wa polisi William Evans wa kikosi cha polisi cha Capitol."Tunatuma salamu za rambirambi kwa familia ya Evans na yeyote anayehuzunika kufuatia kifo chake."- Biden amesema kwenye taarifa.

Maeneo hayo ya majengo ya bunge yamefungwa na usalama kuimarishwa, Ambapo kwasasa Maafisa wa usalama wamesema wameanzisha uchunguzi dhidi ya kisa hicho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.