Star Tv

Rais wa Marekani Joe Biden amesema Vladimir Putin atajuta kwa juhudi zake za kujaribu kushawishi uchaguzi wa urais wa mwaka wa 2020 nchini Marekani kwa niaba ya Donald Trump.

Ripoti ya ujasusi ya Marekani iliyotolewa Jumanne wiki hii inaunga mkono shutuma za muda mrefu kwamba baadhi ya maafisa wa jeshi wa Donald Trump walishirikiana na Urusi kwa kuongeza mashtaka kutoka kwa maafisa wa Ukraine wenye uhusiano wa karibu na Moscow dhidi ya mpinzani wa wakati huo Joe Biden kutoka chama cha Democratic, kabla ya uchaguzi wa mwezi Novemba 2020.

Kwa upande wake Urusi imesema madai hayo hayana msingi wowote na kuyaeleza madai ya idara za upelelezi za Marekani kuwa siyo ya kweli.

Ripoti ya ujasusi ya Marekani iliyotolewa imeongeza maelezo mengine kwenye tuhuma kuwa baadhi ya maafisa waandamizi wa Trump walijaribu kushirikiana na Urusi kwa kusisitiza madai yaliyotolewa dhidi ya aliyekuwa wakati huo mgombea Joe Biden na viongozi wa Ukraine wenye mahusiano na Urusi kuelekea uchaguzi wa Novemba 3.

Ubalozi wa Urusi nchini Marekani umesema katika taarifa kuwa waraka uliotayarishwa na idara ya ujasusi ya Marekani ni tuhuma nyingine zisizo na msingi dhidi ya Urusi kwa kuingilia michakato ya kisiasa ya ndani ya Marekani.

Imesema hakuna maelezo na ushahidi uliotolewa kuthibitisha tuhuma hizo.

Duru tatu zimesema kuwa Marekani inatarajiwa kuiwekea vikwazo Urusi katika siku chache zijazo kwa sababu ya tuhuma hizo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.