Star Tv

Watu nane wakiwemo wanawake wenye asili ya bara Asia wameuawa katika ufyatuaji risasi jimboni Georgia nchini Marekani.

Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa mauaji hayo wakati Korea Kusini ikidai waathirika wanne kati yao walikuwa na asili ya Korea.

Mwanaume mwenye umri wa miaka 21 anashikiliwa kwa tuhuma za kuhusika na mashambulizi yote.

Aidha bado sababu za kutekelezwa kwa shambulizi hilo hazijabainika.

Hata hivyo,uhalifu wa chuki dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Asia umeongezeka zaidi katika miezi ya hivi karibuni ukichochewa na shutuma za kusambaza virusi vya Covid-19.

Katika hotuba yake wiki iliyopita, Rais Joe Biden alilaani uhalifu mbaya wa chuki dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Asia ambao wameshambuliwa, kunyanyaswa, kulaumiwa na kupuuzwa.

ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.